Lugha na Sarufi
Sajili Ya Simu.
Hii ni lugha inayotumiwa katika mazungumzo ya simu.
Sifa za lugha ya simu
Mazungumzo ya simu ni mafupi, hutumia sentensi fupi zenye muundo rahisi.
Hoja hutajwa moja kwa moja bila maneno mengi kwani ili kudhibiti gharama ya simu
Huwa na kukatizana kwa maneno kati ya wazugumzaji.
Huwa ni mazungumzo baina ya watu wawili pekee; anayepiga na anayepokea.
Hutumia istilahi maalum za lugha ya simu kama neno ‘hello’
Huchanganya ndimi (kutumia maneno yasiyo ya lugha nyinginezo) ili kuwasilisha ujumbe kwa upesi.
Ni lugha ya kujibizana.