Ushairi
Penzi wangu usijali.

Maisha hapa chuoni, ni magumu mno sana
Nafunga yangu machoni, ili kesho kuiona
Sembe sukuma mezani, kutia tukizi sana
Penzi wangu usijali nilikwacha nijikimu
Nguo moja nimekita, sio eti ninapenda
Hata nywele sijikata, juu juu zinapanda
Nyayo kwako nimekata, taniua nishakonda
Penzi wangu usijali, nilikwacha nijikimu
Kazi yake muhazili, sitaweka hata chapa
Kwa rehema za Jalali, hitatupwa kwebye pipa
Kwa hakika sina hali, ni maisha nanichapa
Penzi wangu usijali, nilikwacha nijikimu
Za kukwenda kwenye mesi, hata kumi mimi sina
Mkopaji kwenda mesi, limekuwa langu jina
Ninajuta hiyo kasi, likwendavyo hilo jina
Penzi wangu usijali, nilikwacha nijikimu
(Malenga ni Kevin Akong’o)