Ushairi
Nitetee Mola Wangu.
Tenzi :: Nitetee Mola Wangu
1 Nitetee Mola wangu
Wewe kimbilio langu
Duniani sina changu
2 Hali yangu vangu vangu
Nikulacho ni kichungu
Nimejawa naukungu
3 Siku ya tatu sijala
Na bado ni masajala
Nakesha kwenye jalala
4 Kuyaokota makopo
Ningeupata mkopo
Au ja kazi ya popo
5 Maisha yangu ni duni
Sina kitu mfukoni
Uzito upo kitwani
6 Muda wote ni majozi
Nacheka yaja machozi
Vitamu kwangu ni njozi
7 Njoo wangu muokozi
Nsije fanya udokozi
Kifo kiwe yangu dozi
(Malenga ni Abuuadillah)