Nampenda.

NAMPENDA😍😍😍
Nimezama mapenzini
Na sitamani kutoka
Nimempenda Fulani
Na yeye ameridhika
Hata mi mnipe nini
Mimi kwake nimefika
Nampenda kwelikweli
Kumuacha abadani
Kumuacha abadani
Nathubutu kutamka
Nyonga mkalia ini
Huyu wangu muhibaka
Amenikaa moyoni
Katu hawezi kutoka
Nampenda kwelikweli
Kumuacha abadani
Amenijaa kichwani
Siachi kumkumbuka
Hata nikiwa ndotoni
Sautiye yasikika
Namuomba RAHMANI
Marengo kutimizika
Nampenda kwelikweli
Kumuacha abadani
Nampa vitu laini
Meno yasije kun’goka
Biriani ya maini
Ale pindi akitaka
Nae kaniganda yani
Hawezi kuchoropoka
Nampenda kwelikweli
Kumuacha abadani
Anipenda si utani
hatamani kuchepuka
Mimi kwake ndie shani
Nanga’ra nanawirika
Pindi akinita hani
Naitika rabaika
Nampenda kweli kweli
Kumuacha abadani
Pole ya yule Fulani
Kwangu alieondoka
Hakwona yangu thamani
Ndio akachoropoka
Nimempata hayuni
Na Mimi ametosheka
Nampenda kweli kweli
Kumuacha abadani
Kuachana abadani
Labda mola akitaka
Nasi twamwomba manani
Upendo kuimarika
Sote tufike ndoani
Kwa uwezo wa rabbuka
Nampenda kwelikweli
Kumuacha abadani
Kalamu nashusha chini
Nimechoka kuandika
Anipende daimani
Katu nisije achika
Mahasidi wa pembeni
Waishie kuumbuka
Nampenda kwelikweli
Kumuacha abadani
(MTUNZI: Bintrasool)