Habari za sasa
Magoha asema shule zaweza kufunguliwa hivi Karibuni.
Waziri wa Elimu nchini Kenya amewaambia wazazi wajitayarishe vilivyo kwani shule zaweza kufunguliwa wakati wowote kuanzia sasa.Magoha alisema maambukizi ya virusi tandavu vya Korona vinaonekana kupungua siku chache zilizopita hivyo wanatazamia wiki tatu zijazo kuona kama asimilia itafikia tano.Ikumbukwe shirika la Afya duniani limesema kwamba hatua madhubuti zinafaa kuchukuliwa kuepuka kufungua biashara na jamii kiujumla kiholela.
Magoha aliyezungumza katika taasisi ya elimu ya Wote katika kaunti ya Makueni aliwashutumu vikali wakuu wa taasisi hizo kwa kukosa kupanga mikakati ya haraka ya ufunguzi wa taasisi za juu ya elimu.Ikumbukwe wizara ya elimu iliwasihi wakuu wa vyuo kupanga mikakati kurejelewa kwa mafunzo iwapo maambukizi yatapungua.