Maadamu umeniacha
MADAMU UMENIACHA.
Mi sijawahi kupenda, kama nilivyo kupenda.
Leo umesha nitenda, tena ukanamba kwenda.
Kumbe mitili ya Punda, ulitaka mi kukonda.
PENZILO SILO LA KWELI, MADAMU UMENIACHA.💋🥀
Unakumbuka mwenyewe, ulipo ni tamkia.
“Nimekupenda mwenyewe, toa hofu maidia.
Hivi wanipa kiwewe, vibaya kunisemea.
PENZILO SILO LA KWELI, MADAMU UMENIACHA.💋🥀
Ni kikumbuka ya nyuma, mabusu kuniptia.
Nina shindwa kusimama, mwili una nyong’onyea.
Kwa kweli inaniuma, kidonda naugulia.
PENZILO SILO LA KWELI, MADAMU UMENIACHA.💋🥀
Imfikiye habari, ye fulani mwana Ali.
Machozi yanitiriri, mwenziwe mi sina hali.
Akapiga msitari, mapenzi kwake muhali.
PENZILO SILO LA KWELI, MADAMU UMENIACHA.💋🥀
Mwenziwe ameniweza, moyoni nimepaniki.
Nimebaki nikiwaza, kumbe alitaka kiki.
Hi ngoma hatoiweza, lazima atiye tiki.
PENZILO SILO LA KWELI, MADAMU UMENIACHA.💋🥀
Sasa najiamulia, kupenda kwake ni basi.
Na nyuma sitorudia, na kwenda kama risasi.
Nako mbali kifikia, natuwa yangu nafusi.
PENZILO SILO LA KWELI, MADAMU UMENIACHA.💋🥀
(MTUNZI: SAID MRUU)