Baba yangu yupo wapi.
***BABA YANGU YUPO WAPI?*** ** * #MTOTO
Yupo wapi baba yangu, mbona sijawahi mwona / Lanipa kizunguzungu, yeo itaitwa yana / Yamenizidi matungu, nomba niweke bayana / Baba yangu yupo wapi, mama naomba nijibu //// *
#MAMA
Kwani umewaza nini, hadi hivyo wauliza / Hapa ndo kwenu nyumbani, kipi kilichokukwaza / Ningependa nibaini, ewe mwanangu #Kazaza / Ewe mwanangu kipenzi, njoo hapa tuyajenge //// *
#MTOTO Hapo kwako ninakuja, ila usipotezee / Swali langu mie moja, nomba unielezee / Nijipatie faraja, ukweli hebu nigee / Baba yangu yupo wapi, nataka nimtambue //// *
#MAMA
Mwanangu kwanza tulia, kipi leo chakusibu / Kwanza uache kulia, cheki unajipa tabu / Wapaswa kuvumilia, utazua masaibu / Kwangu unakosa nini, kipi ambacho hupati //// *
#MTOTO
Ninakula ninashiba, sivyo maisha yalivyo / Napenda ‘mjue baba, kama vile ‘kujuavyo / Fuadi nina uhaba, najiona ovyoovyo / Baba yangu yupo wapi, ninataka mfahamu //// *
#MAMA
Ukikua utajua, kwanini hivi twaishi / Mwenyewe utagundua, ukweli na si uzushi / Kisha utayaamua, machungu ima fuleshi / Mwanangu kua uone, wakubwa tunavyoishi //// *
#MTOTO
Mama ninacho kifua, japo mdogo kiumri / Ukweli nataka jua, kujuza yako hiari / Siku nikija tusua, nijue wa kusitiri / Mama yangu nakupenda, hakika wewe shujaa //// *
#MAMA
Babako alikimbia, kisa mie sina kazi / Alisepa ukilia, yamemshinda malezi / Hawezi kuhudumia, maisha magumu shazi / Nduguze siwafahamu, hakutaka niwajue //// *
#MTOTO
Pole mama’ngu jasiri, unileae kwa tabu / Kwa jaala ya Jabari, twaishi hatuharibu / Sasa nimeshaabiri, umenifunza adibu / Ngoja nikateke maji, wewe nenda ukalale //// ** *
(Malenga ni Bin Omary)